Saturday, August 1, 2009

VIJANA NA SIASA

Mimi nilijitosa mapema sana kwenye siasa, hivyo leo ningependa kuwahamasisha vijana ni wakati muafaka kujiingiza kwenye siasa na kugombea nafasi za uongozi mbali mbali ili tuweze kusaidia taifa letu, tusijiulize Taifa linafanya nini kwa ajili yetu bali sisi tunafanya nini kwa ajili ya taifa letu……
Kuna viongozi wengi ambao umri wao ni mdogo lakini wana uwezo mkubwa wa kiutendaji na kuleta mabadiliko kwenye jamii, hivyo vijana ambao ndio taifa la kesho wasisite na wakaanza kuwa Taifa la Leo…